Headlines za wanasoka wa kibongo
kuulizwa kuhusu lini watastaafu kucheza soka zimekuwa zikiandikwa sana
mitandaoni na hata kwenye vyombo vya habari, alianza kusikika nahodha wa
timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars na klabu ya Dar Es Salaam Young African Nadir Haroub Canavaro kuwa kacheza kwa muda mrefu, hivyo lini atastaafu?
Canavaro kupitia
gazeti la habari leo alijibu kuwa kuhusu suala la kustaafu kucheza timu
ya taifa anaweza kufikiria baada ya miaka mitatu, lakini kama atafanya
hivyo ataendelea kuichezea klabu yake ya Yanga kama kawaida. Baada ya hapo millardayo.com ilipata bahati ya kukutana na Abdi Kassim Babi na kumuuliza kama ana mipango ya kuustafu?

Canavaro
“Muda
wa kustaafu haujafika, nafikiria kufanya hivyo baada ya miaka mitatu na
nikistaafu bado nitaendelea na kuichezea Yanga, na ikitokea nimeondoka
Yanga basi ndio mwisho wa jina langu kusikika kwenye soka, kwani
sifikirii kuichezea timu nyingine baada ya hapo,” >>> Canavaro

Abdi Kassim Babi wa pili kutoka kulia akiwa na waamuzi pamoja na nahodha mwenzake wa timu pinzani.
Babi ambaye amewahi kuvitumikia vilabu vya Mtibwa Sugar, Yanga na Azam FC kwa sasa anacheza soka katika klabu ya UiTM ya Malaysia na yupo likizo Tanzania baada ya msimu wa Ligi Kuu Malaysia kumalizika. Majibu Babi ndio haya kuhusu mipango yake ya kuustaafu soka.
0 comments :
Post a Comment