SIJUI KAMA HAYA YANATOKEA BAAADA YA MHESHIMIWA RAIS KUKATAZA BAADHI YA SAFARI ZA MAWAZIRI NJE YA NCHI

NAIBU WAZIRI: Mheshimiwa umepata tarifa za mkutano wa mawaziri utakaofanyika Ujerumani wiki hii ?
WAZIRI: Ndio nimesikia, inatakiwa kwenda maana nimhimu sana.
NAIBU WAZIRI: Unaenda wewe au niende mimi ?
WAZIRI: Nitaenda mimi maana nina mambo mengi sana ya kujadiliana na wenzetu wa nchi mbalimbali ili tupate suluhu la matatizo ya wizara yetu.
NAIBU WAZIRI: Sawa mkuu, basi jiandae uende naamini utarudi na mambo mengi ya msingi.
WAZIRI: Sawa, ngoja nikamuage mheshimiwa Rais.
>>>>Waziri anaingia kwenye gari lake kuelekea magogoni kwenye Ikulu ya nchi kwa mazunguzo na mheshimiwa Rais.
RAIS: OOOh karibu mheshimiwa .
WAZIRI: Asante sana mkuu.
RAIS: Kumbuka lakini nchi haina hela hivyo hata maji tu leo hakuna, au umeshakula kwako ?
WAZIRI: Usijali mkuu nimekula tayari.
kisha anacheka kidogo.
RAIS: Umekula kwako au hela za wizarani ??
WAZIRI: Nimekula kwa ndugu yangu mmoja maana hata familia yangu pia haina hela kama serikali.
Rais anacheka kidogo, kisha anakaa kimya kuashiria waziri anaweza kuendelea na maongezi yaliyompeleka Ikulu.
WAZIRI: Mkuu, kuna mkutano mkubwa unafanyika Ujerumani wiki hii unahusu wizara yangu na ni mhimu sana kuhudhuria, ningependa kukuaga niende kwa maslahi ya taifa.
>>>Rais anaonekana kuchukia kidogo kisha anaongea.
RAIS: Nilishasemaje kuhusu safari za nje ? au nikufute kazi mara moja ?
>>>>Waziri inamchukua muda kueleza umhimu wa ule mkutano mpaka Rais anamwelewa, kisha Rais akainuka na kufungua kabati akachukua simu ya kiganjani na kumpatia waziri.
RAIS: Shika hii simu uunge kifurushi cha international (cha kimataifa) umalizane nao hapa hapa.
>>>>Waziri akiwa bado anashangaa maamzi yale anakumbana na swali toka kwa mheshimiwa Rais.
RAIS: Au huna namba ya waziri wa nchi yeyote aliyehudhuria umwambie arecord clips akutumie kwa whatsap nawe umchangie kwa whatsaap ?
>>>>Waziri inambidi awe mpole anasema sina.
Kisha Rais anafungua komputa na kumwambia waziri atumie mtandao wa skype kuwasiliana na mawaziri walioko ujerumani.
>>>>Waziri anajifanya kuchunguza simu yake kisha anaongea.
WAZIRI: Mkuu nimepata taarifa mpya wanasema mawaziri wote wahudhuri isipokuwa wa Tanzania.
RAIS: Hayo ndio mambo ya msingi, hebu fikiria mkiondoka ziara za kustukiza atafanya nani kwenye wizara yenu ?
>>>>Waziri anaamua kuaga na kuondoka kurudi ofisini kwake na kumkuta naibu waziri wake.
WAZIRI: Mkuu anasema tuunge kifurushi cha international tumalizane na walioko Ujerumani kwa simu !
NAIBU WAZIRI: Najua mkuu yeye hana udhoefu na masuala ya international affairs ndio maana anaogopa sana nje.
>>>>Kisha naibu waziri anajishtukia anauliza "Au unanirecord mheshimiwa ?"
WAZIRI: Siwezi kufanya utoto huo.
>>>>Naibu waziri anaendelea.
NAIBU WAZIRI: Unajua nje alienda mara moja tu mwaka 2003 alipodondoka Bungeni akapelekwa India, tatizo lake la moyo huwa linamsumbua hata akikaa kwenye ndege muda wa masaa mawili tu.
WAZIRI: Ngoja tusijihangaishe tule mshahara tu na kuzunguka na waandishi wa habari kila sehemu tumlidhishe .
Share on Google Plus

About KAKSIGABA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment