Dr Slaa amesema hivi katika ukurasa wake wa jamiiforum
"Siasa ya unafiki sipendi. Nimenyamaza lakini naona mnazidi kunichokoza.
Ni afadhali mngelikaa kimya kama nilivyonyamaza mimi. Uwongo wowote na
upotoshwaji wowote sitauvumilia. Nitaukanusha hapo hapo. Hata kama una
lengo lako ambalo silifahamu naomba sana usitumie jina langu.
Nimefundishwa uwongo ni dhambi siko tayari kushiriki dhambi hiyo.
sina kikao chochote cha Secretariat sina mpango wowote ninaopanga
kuwasilisha popote. Naomba watanzania wapuuze propaganda zote
zinazofanyika kwa jina langu.
Ningehitaji kutuma taarifa yoyote kwa umma ningeliita Press Conference
Mwenyewe au ningelitumia utaratibu wowote uliouliozoeleka.
Naomba kutoa onyo kwa mtu yeyote awaye, matumizi ya jina la Dr Slaa yakome."
taarifa hii inafuatia taarifa zilizosambazwa na mmoja wa wanachadema aitwaye Yericko Nyerere aliyeandika hivi
" Jioni ya leo Dr. Slaa katibu mkuu wa CHADEMA atawasilisha
mpango mkakati wa ushindi mbele ya sekretariet tayari kuelekea cc
kesho.
Hatua hiyo inafuatia jopo la wataalamu nane likiongozwa na Dr Slaa
kujichimbia kwa wiki nzima kuhariri na kuchakata taarifa mbalimbali za
umoja wa vikosi kazi vya vyama vinavyounda UKAWA,
Japo maneno na uzushi mwingi umezagaa mitaani lakini Dr hayumbishwi na
hilo, mida ya usiku wa leo atawasilisha ripoti hiyo katika vikao
vinavyofanyika kwa siri kubwa ili kuepuka maadui ambao kwasasa
tunapigana vita nao usiku na mchana.
Kesho ndio rasmi Dr. Slaa atawasilisha mbele ya cc mipango mkakati hiyo ikiwemo Ilani nk.
Pipoooooooz!!!!"
Home
/
HABARI
/
RANDOM POSTS
/
SIASA
/
Slider
/
Dr slaa akanusha taarifa za upotoshaji zinazotolewa na viongozi wa chadema kumhusu yeye
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments :
Post a Comment