NITAISHINDAJE DHAMBI INAYONITESA? Na
Mtumishi Peter Mabula. Ni ujumbe alioniandikia ndugu mmoja ambaye alihitaji
msaada wa kiroho. Ndugu huyu alianiandikia hivi; Hallo Peter Mabula mtumishi wa
MUNGU. kwanza namshukuru MUNGU kwa kuyapitia mafundisho yako, kwani kwa muda
mrefu nimekuwa nikifikiria njia ya kuacha uzinzi kwani sioni FAIDA yake lakini
kila nikijitahidi kuacha najikuta nimetumbukia tena na moyo unaniuma sana kwani
nilikuwa NIMEOKOKA na kwa kweli nilikuwa na matamanio mkubwa ya kumtumikia
Mungu na sasa hayapo kabisa na kwa kweli uvivu katika kumtafuta Mungu mara kwa
mara umenifanya nirudi nyuma na kila nkijitahidi kusimama najikuta narudi nyuma
kweli inaniumiza Imefika mahali nimekata tamaa kabisa hata ya kwenda kanisani
na hata nikitamani kwenda kanisani nakuta moyo unanirudisha ; Na isitoshe kila
nikifikiria maovu niliyomtenda Mungu naona kabisa kama sina nafasi kwake, kwa
mtu niliyemjua na kuanza kutenda maovu mabaya ingawa natamani sana nirudi kwake
Na mbaya zaidi kweli wakati mwingine nimekuwa nikiomba maombi kwa watumishi wa
MUNGU kuomba sala ya toba lakini najikuta narudi tena kulekule hivyo naona kama
namtania Mungu na kuingia kanisani nkiwa mwenye dhambi naona kama kumfanyia
masihara muumba naomba ushuri wako. Baada ya mimi Peter Kuusoma ujumbe wa ndugu
huyo hapo juu nilimjibu na kuahidi kuanza kumuombea. Majibu yangu hayo nataka
yakusaidie na wewe ili umpokee BWANA YESU na kusimama imara katika wokovu wa
BWANA. Majibu yangu ni haya; ubarikiwe kwa kunieleza siri yako inayokutesa kwa
muda mrefu. Naomba nikushauri kama ifuatavyo; Kuacha dhambi kwa mtu yeyote huja
baada ya mtu huyo kuamua kuipenda mbingu badala ya jehanamu. Ukijua kwamba kuna
ziwa la moto ambalo waovu wataenda huko milele basi utakuwa na sababu kuu ya
kuamua kubadilika. ''Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu
cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.-Ufunuo 20:15'' Biblia iko wazi
kabisa juu wa watenda dhambi wasio tubu kwamba kuna ziwa la moto. Nakuomba kama
hilo kanisa ambalo uliokokea mwanzo liko karibu basi muone mchungaji na mweleze
kisha atakuongoza sala ya toba na utaanza upya na BWANA YESU. ''Ungameni dhambi
zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa. Kuomba kwake mwenye haki
kwafaa sana, akiomba kwa bidii.-Yakobo 5:16 '' Kama uko mkoa mwingine au uko
mbali na huko basi tafuta kanisa la kiroho kisha amua tu kuokoka kwa upya.
Kulikwepa kanisa hakuwezi kukusaidia kitu chochote. Kumuonea aibu MUNGU kwa
kulikimbia kanisa lake ni kuonea aibu uzima wa milele. ''Kwa sababu, ukimkiri
YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU
alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata
haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila
amwaminiye hatatahayarika.-Warumi 10:9-11'' Binafsi nitakuombea juu ya MUNGU
kukusaidia katika hilo jambo lakini pia maamuzi ya jinsi ya kuishi yako kwako
mwenyewe. Wengi husema vishawishi ndivyo vilivyowapelekea kufanya dhambi,
wengine husema ujana na wengine husema shetani lakini mimi nakuambia kwamba
mhusika mwenyewe ndio huwa chanzo cha uovu wake. Yohana 3:18-21 '' Amwaminiye
yeye(YESU) hahukumiwi; asiyeamini amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini
jina la Mwana pekee wa MUNGU. Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja
ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa
maovu. Maana kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru,
matendo yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili
matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU.'' Kama ukiambiwa
chakula kilicho mbele yako kina sumu hakika hutakula hata kama ni kwa
kulazimishwa hutakubali. dhambi ni mbaya kuliko sumu maana dhambi inaweza kuzaa
jehanamu hivyo kama tunaiogopa sumu kwenye chakula basi tuogope na dhambi kwa
namna hiyo hiyo maana dhambi ina madhara makubwa sana zaidi ya sumu. Nakuomba
okoka kwa upya kisha fanya yafuatayo; 1. Jitenge na marafiki wabaya
waliokusaidia mwanzo wewe kuingia dhambini. 2. Hakikisha unakuwa mhudhuliaji wa
kila kipindi cha ibada kanisani kuanzia katikati ya wiki na jumapili pia. 3.
Tendea kazi Neno la MUNGU unalofundishwa kanisani. 4. Uwe muwazi kwa baba yako
wa kiroho ili akusaidie kwa ushauri na maombi. 5. Jiunge na kundi la maombi
kanisani na hakikisha unakuwa muombaji maana kazi mojawapo ya maombi ni
kututiisha mwili ili tamaa zisikusumbue. 6. Amua kuwa kiumbe kipya kisicho
husika na dhambi maana ukiwa na nia hiyo ROHO MTAKATIFU atakuja kwako na
kukusaidia jinsi ya kuishi ili ubaki katika utakatifu. 7. Jiunge na huduma
kanisani ili jambo hilo likusaidie kuwa busy na huduma na kwa kuwa kwenye
huduma kutakusaidia wewe kuwa kwenye mtandao mkubwa wa kuombewa mara kwa mara
na wana kanisa. Mfano ukijiunga na kwaya itakuwa kwako rahisi kuombewa maana
wanaoombea huduma za kanisani ni wengi. 8. Sahau mambo ya nyuma na yafute
kabisa kwenye akili yako ili yasikufanye ukose ujasiri wa kuendelea mbele. 9.
Hakikisha unakuwa kielelezo cha matendo mema. 10. Liishi Neno la MUNGU siku
zote. Mathayo 13:41-43 '' Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao
watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao maasi, na
kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno. Ndipo
wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa BABA yao. Mwenye masikio, na
asikie. '' Ndio maana Biblia siku zote inatushauri kwamba ''Tubuni basi,
mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako
kwake Bwana;-Matendo 3:19'' Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo
la kwanza la MUNGU ni wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba
tubu na okoka. Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo
kuishi maisha matakatifu ya wokovu. Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha
yako yamejaa dhambi nakuomba okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako , nakusihi
sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia kuna uzima wa
milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu. MUNGU wangu akubariki
sana na akupe ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe ufahamu wa kuliishi
kusudi lake jema kwako. ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo yangu. Ni mimi
ndugu yako Peter M Mabula. 0714252292. mabula1986@gmail.com Ubarikiwe sana kwa
kusoma somo hili.
NITAISHINDAJE DHAMBI
INAYONITESA?
Na Mtumishi Peter Mabula.
Ni ujumbe alioniandikia ndugu mmoja ambaye alihitaji msaada wa kiroho.
Ndugu huyu alianiandikia hivi;
Hallo Peter Mabula mtumishi wa MUNGU.
kwanza namshukuru MUNGU kwa kuyapitia mafundisho yako, kwani kwa muda
mrefu nimekuwa nikifikiria njia ya
kuacha uzinzi kwani sioni FAIDA yake lakini kila nikijitahidi kuacha
najikuta nimetumbukia tena na moyo unaniuma sana kwani nilikuwa
NIMEOKOKA na kwa kweli nilikuwa na matamanio mkubwa ya kumtumikia
Mungu na sasa hayapo kabisa na kwa kweli uvivu katika kumtafuta Mungu
mara kwa mara umenifanya nirudi nyuma na kila nkijitahidi kusimama
najikuta narudi nyuma kweli inaniumiza
Imefika mahali nimekata tamaa kabisa hata ya kwenda kanisani na
hata nikitamani kwenda kanisani nakuta moyo unanirudisha ;
Na isitoshe kila nikifikiria maovu niliyomtenda Mungu naona kabisa
kama sina nafasi kwake, kwa mtu niliyemjua na kuanza kutenda maovu
mabaya ingawa natamani sana nirudi kwake
Na mbaya zaidi kweli wakati mwingine nimekuwa nikiomba maombi kwa
watumishi wa MUNGU kuomba sala ya toba lakini najikuta narudi tena
kulekule hivyo naona kama namtania Mungu na kuingia kanisani nkiwa
mwenye dhambi naona kama kumfanyia masihara muumba naomba ushuri wako.
Baada ya mimi Peter Kuusoma ujumbe wa ndugu huyo hapo juu nilimjibu na
kuahidi kuanza kumuombea. Majibu yangu hayo nataka yakusaidie na wewe
ili umpokee BWANA YESU na kusimama imara katika wokovu wa BWANA.
Majibu yangu ni haya;
ubarikiwe kwa kunieleza siri yako inayokutesa kwa muda mrefu.
Naomba nikushauri kama ifuatavyo;
Kuacha dhambi kwa mtu yeyote huja baada ya mtu huyo kuamua kuipenda
mbingu badala ya jehanamu.
Ukijua kwamba kuna ziwa la moto ambalo waovu wataenda huko milele basi
utakuwa na sababu kuu ya kuamua kubadilika.
''Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima,
alitupwa katika lile ziwa la moto.-Ufunuo 20:15''
Biblia iko wazi kabisa juu wa watenda dhambi wasio tubu kwamba kuna ziwa
la moto.
Nakuomba kama hilo kanisa ambalo uliokokea mwanzo liko karibu basi muone
mchungaji na mweleze kisha atakuongoza sala ya toba na utaanza upya na
BWANA YESU.
''Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa.
Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.-Yakobo 5:16 ''
Kama uko mkoa mwingine au uko mbali na huko basi tafuta kanisa la kiroho
kisha amua tu kuokoka kwa upya.
Kulikwepa kanisa hakuwezi kukusaidia kitu chochote.
Kumuonea aibu MUNGU kwa kulikimbia kanisa lake ni kuonea aibu uzima wa
milele.
''Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na
kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa
maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata
kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye
hatatahayarika.-Warumi 10:9-11''
Binafsi nitakuombea juu ya MUNGU kukusaidia katika hilo jambo lakini pia
maamuzi ya jinsi ya kuishi yako kwako mwenyewe.
Wengi husema vishawishi ndivyo vilivyowapelekea kufanya dhambi, wengine
husema ujana na wengine husema shetani lakini mimi nakuambia kwamba
mhusika mwenyewe ndio huwa chanzo cha uovu wake.
Yohana 3:18-21 '' Amwaminiye yeye(YESU) hahukumiwi; asiyeamini
amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa
MUNGU. Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu
wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. Maana
kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo
yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili
matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU.''
Kama ukiambiwa chakula kilicho mbele yako kina sumu hakika hutakula hata
kama ni kwa kulazimishwa hutakubali.
dhambi ni mbaya kuliko sumu maana dhambi inaweza kuzaa jehanamu hivyo
kama tunaiogopa sumu kwenye chakula basi tuogope na dhambi kwa namna
hiyo hiyo maana dhambi ina madhara makubwa sana zaidi ya sumu.
Nakuomba okoka kwa upya kisha fanya yafuatayo;
1. Jitenge na marafiki wabaya waliokusaidia mwanzo wewe kuingia
dhambini.
2. Hakikisha unakuwa mhudhuliaji wa kila kipindi cha ibada kanisani
kuanzia katikati ya wiki na jumapili pia.
3. Tendea kazi Neno la MUNGU unalofundishwa kanisani.
4. Uwe muwazi kwa baba yako wa kiroho ili akusaidie kwa ushauri na
maombi.
5. Jiunge na kundi la maombi kanisani na hakikisha unakuwa muombaji
maana kazi mojawapo ya maombi ni kututiisha mwili ili tamaa
zisikusumbue.
6. Amua kuwa kiumbe kipya kisicho husika na dhambi maana ukiwa na nia
hiyo ROHO MTAKATIFU atakuja kwako na kukusaidia jinsi ya kuishi ili
ubaki katika utakatifu.
7. Jiunge na huduma kanisani ili jambo hilo likusaidie kuwa busy na
huduma na kwa kuwa kwenye huduma kutakusaidia wewe kuwa kwenye mtandao
mkubwa wa kuombewa mara kwa mara na wana kanisa. Mfano ukijiunga na
kwaya itakuwa kwako rahisi kuombewa maana wanaoombea huduma za kanisani
ni wengi.
8. Sahau mambo ya nyuma na yafute kabisa kwenye akili yako ili
yasikufanye ukose ujasiri wa kuendelea mbele.
9. Hakikisha unakuwa kielelezo cha matendo mema.
10. Liishi Neno la MUNGU siku zote.
Mathayo 13:41-43 '' Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao
watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao
maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na
kusaga meno. Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa
BABA yao. Mwenye masikio, na asikie. ''
Ndio maana Biblia siku zote inatushauri kwamba
''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za
kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;-Matendo 3:19''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni
wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na
okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi
maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba
okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako ,
nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia
kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.
Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
NITAISHINDAJE DHAMBI
INAYONITESA?
Na Mtumishi Peter Mabula.
Ni ujumbe alioniandikia ndugu mmoja ambaye alihitaji msaada wa kiroho.
Ndugu huyu alianiandikia hivi;
Hallo Peter Mabula mtumishi wa MUNGU.
kwanza namshukuru MUNGU kwa kuyapitia mafundisho yako, kwani kwa muda
mrefu nimekuwa nikifikiria njia ya
kuacha uzinzi kwani sioni FAIDA yake lakini kila nikijitahidi kuacha
najikuta nimetumbukia tena na moyo unaniuma sana kwani nilikuwa
NIMEOKOKA na kwa kweli nilikuwa na matamanio mkubwa ya kumtumikia
Mungu na sasa hayapo kabisa na kwa kweli uvivu katika kumtafuta Mungu
mara kwa mara umenifanya nirudi nyuma na kila nkijitahidi kusimama
najikuta narudi nyuma kweli inaniumiza
Imefika mahali nimekata tamaa kabisa hata ya kwenda kanisani na
hata nikitamani kwenda kanisani nakuta moyo unanirudisha ;
Na isitoshe kila nikifikiria maovu niliyomtenda Mungu naona kabisa
kama sina nafasi kwake, kwa mtu niliyemjua na kuanza kutenda maovu
mabaya ingawa natamani sana nirudi kwake
Na mbaya zaidi kweli wakati mwingine nimekuwa nikiomba maombi kwa
watumishi wa MUNGU kuomba sala ya toba lakini najikuta narudi tena
kulekule hivyo naona kama namtania Mungu na kuingia kanisani nkiwa
mwenye dhambi naona kama kumfanyia masihara muumba naomba ushuri wako.
Baada ya mimi Peter Kuusoma ujumbe wa ndugu huyo hapo juu nilimjibu na
kuahidi kuanza kumuombea. Majibu yangu hayo nataka yakusaidie na wewe
ili umpokee BWANA YESU na kusimama imara katika wokovu wa BWANA.
Majibu yangu ni haya;
ubarikiwe kwa kunieleza siri yako inayokutesa kwa muda mrefu.
Naomba nikushauri kama ifuatavyo;
Kuacha dhambi kwa mtu yeyote huja baada ya mtu huyo kuamua kuipenda
mbingu badala ya jehanamu.
Ukijua kwamba kuna ziwa la moto ambalo waovu wataenda huko milele basi
utakuwa na sababu kuu ya kuamua kubadilika.
''Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima,
alitupwa katika lile ziwa la moto.-Ufunuo 20:15''
Biblia iko wazi kabisa juu wa watenda dhambi wasio tubu kwamba kuna ziwa
la moto.
Nakuomba kama hilo kanisa ambalo uliokokea mwanzo liko karibu basi muone
mchungaji na mweleze kisha atakuongoza sala ya toba na utaanza upya na
BWANA YESU.
''Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi, na kuombeana, mpate kuponywa.
Kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana, akiomba kwa bidii.-Yakobo 5:16 ''
Kama uko mkoa mwingine au uko mbali na huko basi tafuta kanisa la kiroho
kisha amua tu kuokoka kwa upya.
Kulikwepa kanisa hakuwezi kukusaidia kitu chochote.
Kumuonea aibu MUNGU kwa kulikimbia kanisa lake ni kuonea aibu uzima wa
milele.
''Kwa sababu, ukimkiri YESU kwa kinywa chako ya kuwa ni BWANA, na
kuamini moyoni mwako ya kuwa MUNGU alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa
maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata
kupata wokovu. Kwa maana andiko lanena, Kila amwaminiye
hatatahayarika.-Warumi 10:9-11''
Binafsi nitakuombea juu ya MUNGU kukusaidia katika hilo jambo lakini pia
maamuzi ya jinsi ya kuishi yako kwako mwenyewe.
Wengi husema vishawishi ndivyo vilivyowapelekea kufanya dhambi, wengine
husema ujana na wengine husema shetani lakini mimi nakuambia kwamba
mhusika mwenyewe ndio huwa chanzo cha uovu wake.
Yohana 3:18-21 '' Amwaminiye yeye(YESU) hahukumiwi; asiyeamini
amekwisha kuhukumiwa; kwa sababu hakuliamini jina la Mwana pekee wa
MUNGU. Na hii ndiyo hukumu; ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu
wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu. Maana
kila mtu atendaye mabaya huichukia nuru, wala haji kwenye nuru, matendo
yake yasije yakakemewa. Bali yeye aitendaye kweli huja kwenye nuru, ili
matendo yake yaonekane wazi ya kuwa yametendwa katika MUNGU.''
Kama ukiambiwa chakula kilicho mbele yako kina sumu hakika hutakula hata
kama ni kwa kulazimishwa hutakubali.
dhambi ni mbaya kuliko sumu maana dhambi inaweza kuzaa jehanamu hivyo
kama tunaiogopa sumu kwenye chakula basi tuogope na dhambi kwa namna
hiyo hiyo maana dhambi ina madhara makubwa sana zaidi ya sumu.
Nakuomba okoka kwa upya kisha fanya yafuatayo;
1. Jitenge na marafiki wabaya waliokusaidia mwanzo wewe kuingia
dhambini.
2. Hakikisha unakuwa mhudhuliaji wa kila kipindi cha ibada kanisani
kuanzia katikati ya wiki na jumapili pia.
3. Tendea kazi Neno la MUNGU unalofundishwa kanisani.
4. Uwe muwazi kwa baba yako wa kiroho ili akusaidie kwa ushauri na
maombi.
5. Jiunge na kundi la maombi kanisani na hakikisha unakuwa muombaji
maana kazi mojawapo ya maombi ni kututiisha mwili ili tamaa
zisikusumbue.
6. Amua kuwa kiumbe kipya kisicho husika na dhambi maana ukiwa na nia
hiyo ROHO MTAKATIFU atakuja kwako na kukusaidia jinsi ya kuishi ili
ubaki katika utakatifu.
7. Jiunge na huduma kanisani ili jambo hilo likusaidie kuwa busy na
huduma na kwa kuwa kwenye huduma kutakusaidia wewe kuwa kwenye mtandao
mkubwa wa kuombewa mara kwa mara na wana kanisa. Mfano ukijiunga na
kwaya itakuwa kwako rahisi kuombewa maana wanaoombea huduma za kanisani
ni wengi.
8. Sahau mambo ya nyuma na yafute kabisa kwenye akili yako ili
yasikufanye ukose ujasiri wa kuendelea mbele.
9. Hakikisha unakuwa kielelezo cha matendo mema.
10. Liishi Neno la MUNGU siku zote.
Mathayo 13:41-43 '' Mwana wa Adamu atawatuma malaika zake, nao
watakusanya kutoka katika ufalme wake machukizo yote, na hao watendao
maasi, na kuwatupa katika tanuru ya moto, ndiko kutakuwako kilio na
kusaga meno. Ndipo wenye haki watakapong'aa kama jua katika ufalme wa
BABA yao. Mwenye masikio, na asikie. ''
Ndio maana Biblia siku zote inatushauri kwamba
''Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za
kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana;-Matendo 3:19''
Naamini kabisa kuna kitu umejifunza, lakini lengo la kwanza la MUNGU ni
wewe uokoke. Kama unaishi maisha ya dhambi ndugu nakuomba tubu na
okoka.
Kama hujampokea YESU nakuomba umpokee leo na uanze kuanzia leo kuishi
maisha matakatifu ya wokovu.
Kama wewe ni mtu wa kanisani lakini maisha yako yamejaa dhambi nakuomba
okoka upya na amua kumpendeza MUNGU kuanzia leo.
Kama wewe umegeuza kanisa kama kichako chako cha kuficha uovu wako ,
nakusihi sana umche MUNGU maana kuna ziwa la moto kwa waovu, lakini pia
kuna uzima wa milele kwa wateule wa KRISTO wanaoishi maisha matakatifu.
MUNGU wangu akubariki sana na akupe
ufahamu wa kumjua yeye na Neno lake, akupe
ufahamu wa kuliishi kusudi lake jema kwako.
ubarikiwe sana pia kwa kujifunza masomo
yangu.
Ni mimi ndugu yako Peter M Mabula.
0714252292.
mabula1986@gmail.com
Ubarikiwe sana kwa kusoma somo hili.
Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
Copy the BEST Traders and Make Money : http://bit.ly/fxzulu
0 comments :
Post a Comment