faru asafirishwa kilomita 16,000 akazalishe
Kifaru dume mmoja amesafirishwa umbali za kilomita 16,000 kutoka Marekani hadi Indonesia ili akazalishe.
Kifaru
huyo kutoka Sumatra, ambaye vifaru wa aina yake wamo katika hatari ya
kuangamia, amekuwa akiishi katika kituo cha kufugia wanyama pori
Marekani.Mnyama huyo aliyepewa jina la Harapan alizaliwa katika kituo cha kufugia wanyama cha Cincinnati, na ndiye kifaru pekee wa Sumatra aliyekuwa amebaki akiishi katika mataifa ya magharibi.
Wahifadhi wa wanyamapori wanatumai atajamiiana na vifaru jike katika mbuga moja ya kitaifa Indonesia.
Harapan mwenye umri wa miaka minane, ambaye jina lake linamaanisha matumaini, alisafirishwa kupitia ardhini, angani na majini hadi hifadhi ya vifaru katika mbuga ya wanyama ya Way Kambas.
Vifaru wa Sumatra ndio wadogo zaidi na ndio pekee kutoka Asia ambao huwa na pembe mbili. Huwindwa sana na majangili kwa sababu pembe zao hutumiwa kutengeneza tiba ya kiasili Uchina.
0 comments :
Post a Comment