PAPA ANAWAAMBIAVIONGOZI KUWA NI VIZURI KUWEKEZA KWA VIJANA KWANI VIJANA NI NGUVU KAZI AMBAYO INAHITAJI KUTUMIKA NANDIO WAJENZI WA TAIFA
PAPA ANASEMA VIONGOZI SERIKALI WATENDE HAKI KWA RAIA WOTE
PAPA ANSEMA KUWA MATUMIZI BORA YA RASILIMALI ZA ASILIAMBAZO MUNGU AMEIJALIA KENYA NDIYO NJIA PEKEE ITAKAYOHAKIKISHA USAWA KENYA, PIA ANASEMA UBINADAMU NA USAWA NI NJIA NZURI YA KUHAKIKISAH KENYA INAFANIKIWA
PAPA ANAANZA KWA KUMSHUKURU RAIS NA WAKENYA KWA UKARIBISHO NA UKARIMU WALIOUONYESHA. ALIPOFIKA
RASI UHURU KENYATA ANAMKARIBISHA PAPA SASA
RAIS ANAMWOMBA PAPA KUMWOMBEA YEYE MWENYEWE NA KENYA ILI MUNGU AWASIKIE
RAIS UHURU KENYATA ANASEMA ELIMU BORA INAYOTOLEWA NA KANISA IMEIFIKISHA KENYA KWENYE MAFANIKIO MAKUBWA. NA ANASEMA YEYE MWENYEWE NI MFANO WA MTU ALIYEFAIDIKA NA ELIMU KATIKA SHULE ZA KANISA KATOLIKI
ANAISHUKURU KANISA KATOLIKI KWA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA KUTOA HUDUMA MBALI MBALI ZA KIJAMII KAMA AFYA NA ELIMU
ANASHUKURU VIONGOZI WA DINI KWA JUHUDI KUBWA WALIYOWEKA KUIJENGA KENYA YENYA UMOJA
ANASEMA PIA WAKENYA WAMEGAWANYWA NA UKABILA NA UDINI
RAIS UHURU KENYATA ANAMSHUKURU BABA MTAKATIFU KWA KUANZA ZIARA YAKE NCHINI KENYA. NA ANAMWELEZA PAPA KUWA WAKENYA WANAYOFURAHA NA MSISIMKO MKUBWA KWANI WANAKABILIWA NACHANGAMOTO KAMA RUSHWA NA UGAIDI. RAIS ANAMWOMBA PAPA KUWAOMBEA WAKENYA KUSHINDA VITA DHIDI YA UFISADI NA UGAIDI
PAPA NA MWENYEJI WAKE BABA MTAKATIFU FRANCIS WANARUDI UKUMBINI
RAIS WA ZAMANI WA KENYA NDUGU DANIEL ARAP MOI ANAINGIA UKUMBINI PAMOJA NA MWAI KIBAKI
PAPA SASA AMEINGIA IKULU YA NAIROBI KWA MAZUNGUMZO NA RAIS UHURU KENYA;BAADA MUDA MFUPI ATAHUTUBIA WAKENYA MOJA KWA MOJA
PAPA SASA ANAPANDA MTI WA KUMBUKUMBU
7:44 Papa Francis anapigiwa mizinga 21 ambayo
kawaida hutumiwa kulaki kiongozi wa taifa jingine. Papa Francis ndiye
kiongozi wa Vatican.
17:40 Papa Francis awasili Ikulu, Nairobi na kulakiwa na Rais Uhuru Kenyatta.
17:28 Rais Kenyatta amewasili ikulu ya Nairobi. Papa Francis yuko njiani kuelekea huko ambapo atakaribishwa rasmi Kenya.
17:25 Hivi ndivyo Papa Francis alivyoandika kwenye kitabu uwanja wa ndege wa JKIA: "na maombi na shukrani kwa kuwatunza wasafiri."
Haya ni kwa mujibu wa Nexus Kenya, idara ya habari ya serikali ya Kenya.
17:15 Papa Francis aingia kwenye gari lake na kuondoka.
16:52 Alakiwa kwa shangwe na nderemo. Amsalimia Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta. 16:50 Wanahabari walioandamana na Papa Francis watangulia kushuka kutoka kwenye ndege. 16:41 Viongozi
wa Kanisa Katoliki wakiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wamejiandaa
kumlaki Papa Francis atakaposhuka kutoka kwenye ndege iliyombebea,
ambayo ni kutoka shirika la ndege la Italia, Alitalia. 16:33 Ndege iliyombeba Papa Francis yatua uwanja wa ndege wa JKIA, Nairobi. 16:25 Ndege iliyombeba Papa Francis kwa sasa imo kwenye anga ya Kenya. 16:25 Rais
Kenyatta ameelekea uwanja wa ndege wa JKIA kumlaki Papa Francis ambaye
anatarajiwa kuwasili wakati wowote baada ya saa kumi unusu alasiri. 16:20 Mabango yamewekwa katika barabara mbalimbali kumkaribisha Papa Francis Kenya 16:08 Papa Francis aandika kwenye Twitter: "Mungu abariki Kenya". 15:07 Papa Francis amezungumza na wanahabari walioandamana naye kwenye safari ya ndege kutoka Roma kuelekea Nairobi. “Ninaenda Kenya, Uganda na kwa ndugu zangu wa
Jamhuri ya Afrika ya Kati nikiwa na furaha,” shirika la habari la
Reuters limemnukuu akisema. Image copyrightAP “Tutumai kuwa ziara hii itazalisha matunda mema, kiroho na kimwili.” Image copyrightReuters 12:36 Huyu hapa ni Papa Francis akiabiri ndege. Ndege yake ishaondoka uwanja wa ndege wa Fiumicino, Roma kuelekea Nairobi Kenya. 12:11 Wakenya wanaendelea kujiandaa
kumpokea Papa Francis baadaye leo. Barabarani na katika majumba, kuna
mabando ya kumkaribisha Papa.
10:33 Ndege ya
Papa Francis imepaa kutoka uwanja wa ndege wa Fiumicino, Roma, ikiwa
imechelewa kwa karibu robo saa. Anatarajiwa kuwasili uwanja wa kimataifa
wa ndege wa Jomo Kenyatta saa 17:00. 10:00
Hujambo! Karibu tukupashe yanayojiri katika ziara ya Papa Francis
barani Afrika ambayo itamfikisha Kenya, Uganda na Jamhuri ya Afrika ya
Kati.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment