WALICHOSEMA VIONGOZI WA CHADEMA/UKAWA NA NDUGU KWENYE MAZISHI ALPHONCE MAWAZO

Jana mamia ya wananchi wa jiji la mwanza walijumuka katika uwanja wa furahisha kwa lengo la kuuaga mwili wa aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa geita Hayati Alphonce Mawazo. Katika Kusanyiko hilo Viongozi wa Kitaifa wa chadema na ndugu jamaa na marafiki wa Marehemu walitoa matamko mbalimbali. baadhi ya matamko hayo ni haya hapa chini;
LOWASA
Amesema polisi wasipochukua hatua kwa waliomuua marehemu Mawazo watajichukulia hatua wao.
“Hawa Polisi wanafanya mambo yao kiimla-imla, kiujanja ujanja, wao wameleta magari ya washawasha yaliyonunuliwa kwa Dola za Kimarekani 282 milioni, hawana namna ya kuyatumia, wameamua kuwachokoza wananchi ili waweze kuyatumia.
Wananchi nawaomba sisi tuache vurugu ili sasa hayo magari yao walionunua tuone watakavyo yatumia, wananunua magari alafu shuleni hakuna madawati na barabara hakuna,” amesema Lowassa.
 MBOWE
“Wananchi wamechoka kuuliwa kama ilivyotokea kwa wafuasi wa Chadema tangu mwaka 2011 mpaka sasa wakati huu wa Mawazo…tumechoka kufa, mwenye akili na afahamu,”
“Kamanda Mkumbo lazima alipe gharama zote za siku nane za kumweka Lowassa, Sumaye, Mbowe na wabunge zaidi ya 50 jijini Mwanza wakisubiri mahakama itende haki na hatimaye kushinda kesi,” amesema mwenyekiti Mbowe.
SUMAYE
“Kamanada Mkumbo lazima alipe gharama zote za siku nane za kumweka Lowassa, Sumaye, Mbowe na wabunge zaidi ya 50 jijini Mwanza wakisubiri mahakama itende haki na hatimaye kushinda kesi,” amesema mwenyekiti Mbowe.
Sumaye amesema Marehemu Mawazo alikuwa akidai haki majukwaani, lakini watu waliotaka kudaiwa haki waliamua kumuua huku vyombo vya dola vikipindapinda ili haki isipatikane kwa amani.
“Lazima tusimamie amani na tupinge kuonewa maana ipo simu moja watu watachoka kuonewa kama ilivyo sasa,”
MTOTO WA MAWAZO PRECIOUS MAWAZO
“Wakati wa uhai wa baba, ndoto yangu ilikuwa niwe mwanasiasa, lakini nitaendelea na hiyo ndoto hadi niwe mwanasiasa mkubwa nchini…katuacha na mdogo wangu akiwa na miaka miwili tunaamini Mungu atatusaidia,”
GODBLESS LEMA
"ukimya wa wananchi katika mauaji wanayofanyiwa, si uoga bali ni unatokana na uchungu walionao, kwani wauaji wakiwa huru hakuna atakayekuwa salama".
MCHUNGAJI SWAI WA KANISA LA THE WINNERS
“Lazima wanadamu wajiulize kwanini vijana wengi wanatumiwa ili kuwaua wengine, tunaiomba serikali iliyopo madarakani isimamie na kukomesha kabisa mauaji yasiyo na hatia,”
"Binadamu hawajaumbwa kwa ajili ya kuuana bali kwa ajili ya kupendana"  
Share on Google Plus

About KAKSIGABA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment