Lakini
akaongeza ubovu wa uwanja, ulichangia kwa kiasi kikubwa wao kushindwa
kucheza soka safi. Katika mechi hiyo, Simba ililazimishwa sare ya bao
1-1 katika dakika za mwisho kabisa.
Akizungumza na SALEHJEMBE, Kerr amesema walikuwa na nafasi kubwa ya kushinda kwa kuwa waliwakamata Toto watakavyo.
“Uliona, tulijitahidi kuwadhibiti na kutawala mchezo, uwanja ulikuwa tatizo katika sehemu kubwa ya mechi hiyo.
“Ilikuwa
vigumu kucheza mpira sahihi kama tulivyopanga. Lakini bado tulikuwa na
nafasi ya kuibuka na ushindi kama tungekuwa makini.
“Mabeki
wetu walishindwa kuwa makini hasa dakika za mwisho na wanajua
tunatakiwa kufanya nini. Bado tuna nafasi ya kupambana, hivyo
tunarekebisha makosa yetu.
“Kawaida unapofanya makosa katika ulinzi, basi watu wanakuadhibu.”
Baada
ya kuibana Toto kwa dakika zote, Simba iliruhusu bao la dakika za
nyongeza baada ya beki Isihaka Hassan kushindwa kuruka juu na kuuwahi
mpira uliomfikia mshambuliaji wa Toto, akafunga kwa ulaini kabisa.
0 comments :
Post a Comment