Nyota
wakubwa duniani katika soka kama David Beckham, Louis Figo, Alexandro
del Piero, Robert Pires, Deco; Dwight Yorke; Andriy Shevchenko na
Roberto Carlos waliungana tena na kucheza mechi pamoja nchini Kuwait.
Ilikuwa mechi maalum kufungua Uwanja wa Jaber Al-Ahmad unaobeba watazamaji 60,000 na watandelea na ziara hiyo katika nchi za Kiarabu.
Pamoja
na Figo na Pires kutupia, lakini mechi hiyo iliisha kwa wakali hao
kulala kwa mabao 4-2 dhidi ya nyota wa Kuwait wanaocheza katika timu
mbalimbali za Ligi Kuu.
KIKOSI CHAO KILIVYOKUWA:
(4-4-2):
Jens
Lehmann; Gianluca Zambrotta, Michel Salgado, Alessandro Nesta, Roberto
Carlos; David Beckham, Luis Figo, Robert Pires, Deco; Dwight Yorke;
Andriy Shevchenko.
Subs: David James, Carles Puyol, Mohamed Aboutrika, Del Piero
Manager: Fabio Capello


0 comments :
Post a Comment