Amesema kazi yao ni kuisimamia Serikali, watakuwa wanapinga kwa hoja za msingi, pia amesema baadhi ya mambo ambayo wao wameyapigia kelele kwa miaka mingi vinatekelezwa sasa na Rais Magufuli, japokuwa sio kwa usahihi.
Amepinga teuzi mbili katika baraza la Mawaziri, amepinga uteuzi wa Waziri wa Katiba na Sheria na uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini Prof. Muhongo kwani wananuka rushwa
Amesema kuwa Dkt. Mwakyembe anahusika na madudu ya bandarini na Bodi ya Bandari iliyovunjwa na Rais Magufuli kwa asilimia kubwa iliteuliwa na Dkt. Mwakyembe.
Pia amesema Prof Muhongo alijiuzulu kwa shinikizo la maazimio ya Bunge, inashangaza anateuliwa hata kabla ya mwaka kukamilika tangu awajibishwe na Bunge.
0 comments :
Post a Comment