Utasikia watu, eti, watumie watu 10 utaingia peponi. Au mambo yako yatakuwa mazuri, hivi mnadhani Pepo mchezo!
Yohana mbatizaj aliishi hadi mapangon kwa kula asali na nzige kwa ajili ya kuitangaza injil,
Mtakatifu Yohana yule mwanafunzi wa Yesu, alikaangwa kwenye mafuta
yanayochemka, baadae akatupwa kwenye kisiwa cha mateso cha patmo mpaka
akafunuliwa mambo mazito na magumu
Isaya aliuwawa kifo cha kukatwa vipandevipande kwa msumeno wa kukatia mbao akiwa hai.
Stephano alipigwa kwa mawe mpaka akafa
Daniel alitumbukizwa kwenye tundu la simba sababu ya kuishindania
imani, Yusuph ilimbidi kwenda gerezani kwa sababu ya kuulinda utakatifu
wake, shedrack, meshack na abelnego walitumbukizwa kwenye tanuru
liwakalo moto. Yote hii ni kwa sababu ya kuisimamia imani
Leo hii
anatokea, mtu, kwa msg yake isiyo na mashiko wala vina alafu
anakutisha, anakulazimisha utume kwa watu 10 maisha yako yatakuwa
mazuri, au eti mm ni Yesu/Mtume Mohammad S.A.W nakuagiza tuma ndani ya
dk 3.
Unadhani mbinguni ni kariakoo? kwa sms yako tu ukale bata
mbingun, halafu unategemea uingie Peponi, tusidanganyane, Pepo sio
mas'hara ndugu yangu, sio maneno matupu na sms nyingi.
Tumche Mungu kisawasawa.
WAKUMBUSHE WANAOGAWA PEPO KWA SMS..😂😂
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments :
Post a Comment