ZAIDI ya nyumba 140 mjini Dodoma zimebomolewa na Mamlaka ya Ustawishaji
Makao Makuu (CDA) kutokana na wananchi kujenga kiholela katika maeneo
yasiyoruhusiwa huku Jeshi la Polisi likilazimika kutumia mabomu ya
machozi kuwatawanya wananchi waliokuwa wakileta fujo ikiwemo kufunga
barabara kuu ya Dodoma – Singida.Bomoabomoa hiyo imefanyika katika
maeneo ya Chinangali, Ndachi, Barabara ya Bahi na Kizota Dampo katika
eneo la Kizota licha ya kutolewa notisi ya siku saba kwa wananchi
hao kuondoka, lakini walikaidi amri hiyo ndipo Jeshi la Polisi pamoja na watendaji wa CDA walianza kazi hiyo.
Hata hivyo, wananchi ambao hawakukubaliana na kazi hiyo, walianza
kuwarushia polisi mawe.Baadhi ya wakazi waliangua vilio wengine
wakipoteza fahamu baada ya kushuhudia nyumba zao
zikibomolewa.Wakizungumza nje ya nyumba zao, baadhi ya wananchi walisema
kazi hiyo ni ya ghafla na hawakupewa taarifa na hawaelewi hatma ya
maisha yao kwani hawana pa kulala.
Mkazi wa Kizota Dampo, Mwajuma
Khamis alisema alikuwa akitegemea nyumba hiyo kwa ajili ya makazi na
sasa hana pa kwenda kufuatia bomoabomoa hiyo.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment