KHAMISI KIIZA; HII SIMBA NI BALAA TUPU


Kutokana na kufanikiwa kuwasajili Brian Majwega, Paul Kiongera na Danny Lyanga, straika Hamis Kiiza wa Simba amesema kikosi chao Image result for kiizakimebadilika na sasa kina mwonekano mpya wa ushindi.

Majwega ni kiungo mshambuliaji kama ilivyo kwa Kiongera wakati Lyanga ni straika, wengine waliosajiliwa na Simba wakati huu ni beki Novatus Lufunga wa African Sports na straika Hija Ugando.

Kiiza raia wa Uganda aliyewahi kuichezea Yanga, amejigamba kuwa ujio wa wachezaji hao utaiongezea nguvu Simba na anaamini pia utamuongezea kasi ya ufungaji.

Hadi sasa Kiiza amefunga mabao nane sawa na Donald Ngoma wa Yanga wakati straika wa Stand United, Elias Maguri akiongoza kwa kufunga mabao tisa katika mechi 11.

Alisema Simba sasa inakuja kivingine kwani usajili uliofanywa umezingatia mahitaji ya timu na mashabiki wategemee mambo mazuri kutoka kwao.
Share on Google Plus

About KAKSIGABA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment