MBWANA SAMATTA NDANI YA TATU BORA ZA WACHEZAJI BORA AFRIKA

Image result for mbwana samata Image result for mbwana samataImage result for mbwana samataMshambulizi matata wa Taifa Stars ya Tanzania na TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mbwana Samatta ametajwa katika orodha ya wachezaji watatu bora na shirikisho la soka la Afrika CAF wanaocheza soka barani Afrika.
Samatta anawania hiyo na wachezaji wengine wawili Baghdad Boundjah wa Algeria na Etoile du Sahel na Kipa machachari wa TP Mazembe ya DR Congo Robert Kidiaba.
Mshindi atachaguliwa na makocha wa timu za taifa na kutangazwa katika dhifa maalum Januari tarehe 7 mwakani.
CAF ilikuwa imewataja wachezaji 37 katika orodha ya awali lakini wakachuja hadi 10 mwezi uliopita.
Share on Google Plus

About KAKSIGABA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments :

Post a Comment