Moshi. Madiwani
wawili wa chama cha demakrasia na maendeleo (Chadema), wanahojiwa na
Polisi mkoani Kilimanjaro kwa tuhuma zinazoangukia katika makosa ya
jinai.
Mmoja wa Madiwani hao kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Rombo, anahojiwa
kwa tuhuma za kutishia kumuua kwa maneno, mbunge wa Jimbo hilo Joseph
Selasini.
Kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro,Flugence Ngonyani,jana
alilithibitishia gazeti la mwananchi kukamatwa kwa madiwani hao kwa
nyakati tofauti na kuhojiwa kisha kuachiwa kwa dhamana
- See more at: http://kusini-tz.blogspot.com/2015/12/madiwani-chadema-mbaroni-kwa-kosa-la.html#sthash.oLVGYUVk.dpuf
Ngonyani alisema Diwani wa kata moja ya wilaya ya Rombo(Jina
linahifadhiwa) alifunguliwa shauri na mbunge Selasini, kwa kile
alichodai kuwa alimtishia kumuua kwa maneno.
Kamanda Ngonyani alisema Mbunge huyo aliandika maelezo ya kuwa Diwani
huyo alitishia kumuua na kwamba upelelezi juu ya tuhuma hizo umeanza.
Pia Diwani mwingine katika Manispaa ya Moshi,nae alishtakiwa kwa kosa la
kumsambulia mkazi wa kata take na kumsababishia majeraha sehemu
mbalimbali za mwili.
Kamanda alisema kuwa uchunguzi unaendelea ili kuweza kubaini kiini
halisi cha ugomvi na kwamba watafikishwa mahakama upelelezi utakapo
kamilika.
Hata hivyo kamanda Ngonyani hakufafanua ni lini matukio hayo yalitokea
zaidi ya kusema Diwani wa Rombo alikamatwa mwishoni mwa wiki na yule wa
Moshi mjini alikamatwa jana.
0 comments :
Post a Comment