Rais John Pombe Magufuli amemfukuza kazi aliyekua Mkurugenzi mkuu wa
Tume ya kuzuia na kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) Ndugu Edward
Hosea kwa kile kilichoelezwa kutoridhishwa na utendaji wa TAKUKURU chini
ya Hosea.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu inasema Magufuli ametengua uteuzi wa Hosea kutokana na kuendelea kushamiri kwa vitendo vya Rushwa nchini bila TAKUKURU kuchukua hatua zinazoridhisha.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu inasema Magufuli ametengua uteuzi wa Hosea kutokana na kuendelea kushamiri kwa vitendo vya Rushwa nchini bila TAKUKURU kuchukua hatua zinazoridhisha.
Kufuatia hatua hiyo Magufuli amemteua aliyekuwa Kamishna Msaidizi wa
Polisi Valentino Mlowola kukaimu Nafasi ya Hosea. Kabla ya uteuzi huo
Kamishna Mlowola alikua Mkurugenzi Msaidizi wa TAKUKURU nafasi
aliyoitumikia kwa siku 12 tu tangu ateuliwe December 5 mwaka huu.
Kabla ya December 5, Mlowola alikua mkuu wa Idara ya Intelijensia ya Jinai ya Jeshi la Polisi, nafasi aliyoitumikia kwa miezi saba tu tangu alipoteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo May mwaka huu.
Kabla ya hapo Mlowola alikua Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza (RPC) tangu mwezi October mwaka jana (2014). Hii ni kusema kuwa ndani ya mwaka mmoja (October 2014 hadi December 2015) Mlowola amepanda vyeo vinne kutoka RPC Mwanza, Kamishna wa Intelijensia jeshi la Polisi, Naibu Mkurugenzi TAKUKURU na sasa Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU.
Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewafukuza kazi viongozi wanne waandamizi wa TAKUKURU kwa kosa la kutotii agizo la Rais na kuamua kusafiri nje ya nchi wakati Rais amezuia safari za nje.
Watumishi hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nictus; ambao wote walisafiri nje ya nchi bila kuomba kibali kwa Rais au Katibu Mkuu Kiongozi.
Taarifa ya Ikulu iliyosomwa na Ombeni Sefue inatoa onyo kwa watumishi wote wa umma kutii agizo la Rais la kutokusafiri nje ya nchi na kama kuna ulazima waombe kibali ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi au kwa Rais mwenyewe.!
Kabla ya December 5, Mlowola alikua mkuu wa Idara ya Intelijensia ya Jinai ya Jeshi la Polisi, nafasi aliyoitumikia kwa miezi saba tu tangu alipoteuliwa na Rais Kikwete kushika wadhifa huo May mwaka huu.
Kabla ya hapo Mlowola alikua Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza (RPC) tangu mwezi October mwaka jana (2014). Hii ni kusema kuwa ndani ya mwaka mmoja (October 2014 hadi December 2015) Mlowola amepanda vyeo vinne kutoka RPC Mwanza, Kamishna wa Intelijensia jeshi la Polisi, Naibu Mkurugenzi TAKUKURU na sasa Kaimu Mkurugenzi Mkuu TAKUKURU.
Katika hatua nyingine Rais Magufuli amewafukuza kazi viongozi wanne waandamizi wa TAKUKURU kwa kosa la kutotii agizo la Rais na kuamua kusafiri nje ya nchi wakati Rais amezuia safari za nje.
Watumishi hao ni Mary Mosha, Ekwabi Mujungu, Doreen Kapwani na Rukia Nictus; ambao wote walisafiri nje ya nchi bila kuomba kibali kwa Rais au Katibu Mkuu Kiongozi.
Taarifa ya Ikulu iliyosomwa na Ombeni Sefue inatoa onyo kwa watumishi wote wa umma kutii agizo la Rais la kutokusafiri nje ya nchi na kama kuna ulazima waombe kibali ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi au kwa Rais mwenyewe.!

0 comments :
Post a Comment