Jupita (Sumbula) ni sayari kubwa ya gesi na pia ni sayari kubwa kuliko zote katika mfumo wetu wa Jua, ina uzito wa asilimia 70% ya uzito wa sayari zote zikijumuishwa. Wanasayansi walipooiita Sumbula kama ni sayari kubwa ya gesi, hawakuipa sifa ya uongo kwani kama ukishuka na parashuti katika uso wa Jupita, unaweza usiguse ardhi ngumu. Katika maelfu ya kilometa unaweza ukawa unakatiza katika tabaka la hewa zito lenye dhoruba, kabla ya kufikia katika uso wa kushangaza wa sayari hiyo wenye bahari (ocean of exotic fluid) ya kina cha kilometa 40,000!
Kwa kutumia darubini ya angani ya Herschel, wanaastronomia wametengeneza ramani yenye pande tatu ya maji katika Sumbula, ambapo wingu la blue linaloizunguka sayari hiyo katika picha ni maji. Kuwepo kwa maji katika Sumbula sio jambo la kushangaza sana, lakini ramani inaonyesha kuwa maji mengi yanapatikana katika kizio cha kusini. Hii iliwashangaza wanaastronomia kwa sababu kama maji yalitoka ndani ya sayari basi walitegemea maji yatawanyike sawa katika pande zote. Kujirundika huku kwa maji katika sehemu moja kunaleta hitimisho moja tu: maji yaliletwa na kimondo cha Shoemaker-levy 9 tu!
0 comments :
Post a Comment