Ndugu wanachama na wapenzi wa Simba kama ambavyo
tutakumbuka ni zaidi ya wiki mbili sasa tangu mchezaji Brian Majegwa
akubaliwe kufanya mazoezi na kikosi cha Simba baada ya kupokea barua
yake ya kuomba kufanya hivyo.
Ni jambo ambalo halifichiki kuwa mchezaji Majwega alionesha dhahiri kupenda kuendelea kuchezea kikosi cha Simba na hivyo ilitulazimu kwanza kumkabidhi kwa benchi la ufundi chini ya kocha wetu Dylan Kerr ili waweze kutupa tathimini kama wangependa Majwega kuendelea kubaki na kikosi cha Simba kikosi cha Simba.
Baada ya kupata ripoti kutoka katika benchi letu la ufundi kuwa kiwango cha Majwega kinaweza kusaidia kikosi cha Simba na kwakuwa mchezaji mwenyewe Majwega alionesha nia ya kutaka kuendelea kubaki na kikosi cha Simba hivyo uongozi wa Simba na uongozi wa Azam FC ulikutana kujadili suala hili na mpaka sasa mazungumzo yanaonesha kuwa kwa asilimia kubwa mchezaji Brian Majegwa atachezea klabu ya Simba baada ya kufungwa kwa dirisha dogo.
Ni imani yetu kuwa mazungumzo yatamalizika vizuri na mchezaji Majwega kuweza kwenda kwenye klabu ambayo anatamani kuichezea kwa sasa.
Imetolewa na
Haji S. Manara
Mkuu wa mawasiliano
SIMBA NGUVU MOJA
Ni jambo ambalo halifichiki kuwa mchezaji Majwega alionesha dhahiri kupenda kuendelea kuchezea kikosi cha Simba na hivyo ilitulazimu kwanza kumkabidhi kwa benchi la ufundi chini ya kocha wetu Dylan Kerr ili waweze kutupa tathimini kama wangependa Majwega kuendelea kubaki na kikosi cha Simba kikosi cha Simba.
Baada ya kupata ripoti kutoka katika benchi letu la ufundi kuwa kiwango cha Majwega kinaweza kusaidia kikosi cha Simba na kwakuwa mchezaji mwenyewe Majwega alionesha nia ya kutaka kuendelea kubaki na kikosi cha Simba hivyo uongozi wa Simba na uongozi wa Azam FC ulikutana kujadili suala hili na mpaka sasa mazungumzo yanaonesha kuwa kwa asilimia kubwa mchezaji Brian Majegwa atachezea klabu ya Simba baada ya kufungwa kwa dirisha dogo.
Ni imani yetu kuwa mazungumzo yatamalizika vizuri na mchezaji Majwega kuweza kwenda kwenye klabu ambayo anatamani kuichezea kwa sasa.
Imetolewa na
Haji S. Manara
Mkuu wa mawasiliano
SIMBA NGUVU MOJA
0 comments :
Post a Comment